Thursday 27 October 2016

WANAFUNZI WAFURAHIA KUWEKWA KWA ALAMA YA PUNDAMILIA BARABARANI ENEO LA CHUO.

NA NAJAT ATHUMANI.
 
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Time school of journalism (Tsj) kilichopo ilala bungoni wemefurahishwa na kitendo cha serikali kuweka kivuko cha alama ya pundamilia kwa waenda kwa miguu  katika barabara kuu ya uhuru waitumiayo kuendea chuoni hapo. 

Aidha mwandishi wetu ameshuhudia uwepo wa alama hiyo ya pundamilia katika eneo hilo na kupata maoni kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho cha uandishi wa habari juu ya kuwepo kwa kivuko hicho.

Mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho Agustino Luambano alifunguka kwa kusema jinsi ya alama ya kivuko hicho kinavyowasaidia hasa katika baadhi ya masomo ambayo wanayasoma BASATA ambapo inawalazimu kuvuka barabara.   

‘‘kwakweli hiki kivuko kimetusaidia sana kwani mwanzo tulikuwa tunapata taabu kuvuka barabara kwa kuhofia magari na pikipiki ambazo huwa zinakwenda kwa kasi sana, sasa tunavuka pasipo shida yoyote” alisema Agustino Luambano mwanafunzi wa chuo.

Naye makamu wa rais wa chuo hicho Fatma Sultani alielezea juhudi walizotumia ili kuwekwa kwa alama hiyo ya kivuko “ tulikuwa tunatamani sana kuwepo kwa kivuko na mara nyingi  tulikuwa tunakaa kikao pamoja na walimu ili watusaidie kufikisha malalamiko yetu sehemu husika  kwani ajali nyingi za wanafunzi kugongwa na magari pamoja na pikipiki zimekuwa zikitokea, nashukuru serikali imesikia kilio chetu  na sasa tunapita kwa amani”. 

Ni wiki kadhaa zimepita ambapo palitokea ajali iliyosababishwa na dereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda kumgonga mwanafunzi wa chuo hicho ajulikanaye kwa jina la HUSNA……. Aliyekuwa akivuka barabara kabla ya kuwekwa kwa alama ya zebra na  kuumizwa vibaya  hivyo kuwahishwa katika hospitali ya wilaya ya ilala Amana kwaajili ya matibabu. Hivyo kuwepo kwa alama hiyo inaaminika kuwa itapunguza ajali za mara kwa mara.
Description: F:\DSC09039.JPG
Kivuko cha alama ya zebra kilichowekwa kwaajili ya  kuwasaidia wanafunzi na wakazi wa eneo la ilala msaada gereji kupita kwa usalama.

Description: F:\DSC09024.JPG
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari  (Tsj) wakiwa wanavuka barabara katika kivuko kuelekea chuoni.

Description: F:\DSC09021.JPG
Wanafunzi wakipita barabarani bila wasiawasi baada ya kuwekwa kwa alama ya kivuko katika eneo hilo.
PICHA NA NAJAT ATHUMANI.

No comments:

Post a Comment